Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali ya Tanzania yapangua ratiba ya masomo
Elimu

Serikali ya Tanzania yapangua ratiba ya masomo

Wanafunzi wakiwa darasani
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kufuta saa 2 za nyongeza za masomo zilizokuwa zinafundishwa kila siku. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Jumatatu tarehe 1 Julai 2020 na Kamishna wa Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Dk. Lyabwene Mtahaba imeelezea sababu za kuondoa saa hizo.

Mabadikiko hayo yametangazwa ikiwa ni siku chache kupita tangu Shule za Msingi na Sekondari kufunguliwa tarehe 29 Juni 2020.

Shule hizo, zilifunguliwa baada ya kufungwa kuanzia tarehe 17 Machi 2020 kutokana na kurupotiwa kwa mgonjwa wa virusi vya corona (Covid-19).

        Soma zaidi:-

Kabla ya kufunguliwa, Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi tarehe 17 Juni 2020 alisema, ili kufidia muda uliopotea kutokana na mapumziko shule zitapaswa kuongeza saa 2 kila siku.

Katika taarifa ya Kamishna wa Elimu, Dk. Mtahaba imesema, imefanya tathimini na kubaini ongezeko hilo la saa 2 kila siku wamebaini haliwezekani.

“Hii ni kutokana na kuwepo kwa shule ambazo kwa sababu mbalimbali zimepewa vibali vya kuendesha masomo kwa mfumo wa ‘double shift’ na pia kutokana na tatizo la usafiri kwa wanafunzi wanaoishi mbali na shule wanazosoma,” amesema Dk. Mtahaba

“Hivyo, wizara inaelekeza shule zirejee kwenye ratiba zao za kawaida za vipindi nane kwa siku,” amesema

Dk. Mtahaba amesema, iwapo uongozo wa shule utaona kuna sababu za msingi za kuongeza muda wa taaluma basi zitumike muda uliopangwa kwenye ratiba ya Shule kwa ajili ya kutekeleza mtaala wa ziada au shughuli za nje ya Darasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!