SERIKALI imepiga marufuku walimu kuwachapa viboko wanafunzi kinyume na utaratibu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Agizo hilo limetolewa leo tarehe 13 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu, William Olenasha, ambapo amesema mwenye ruhusa ya kumchapa mwanafunzi viboko ni mkuu wa shule tena kwa sababu maalum.
“Marufuku mwalimu kumchapa mwanafunzi kinyume na utaratibu, marufuku mwalimu kuonekana akitembeea na kiboko kwa lengo la kumchapa mwanafunzi ni kinyume na sheria,” amesema.
Olenasha ametoa agizo hilo wakati akijibu swali la mbunge viti maalum, Rose Tweve aliyehoji mikakati ya serikali katika kuhakikisha uwepo wa ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Leave a comment