SERIKALI ya Tanzania imesema inafanya mkakati wa kuhakikisha watanzania wote wanaougua magonjwa ya damu watibiwe ndani ya nchi kwa kujengea uwezo hospitali zote nchini. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Mganga Mkuu wa serikali Prof. Muhammad Bakari amesema magonjwa hayo ni kama SeliMundu, Upungufu wa damu na Kansa ya damu.
Amesema kuwa lengo la kufanyika kwa mafunzo hayo ni kuhakikisha kunakuwepo na uwezo wa kutibu wagonjwa ndani ya nchi unaimarika.
“Kinachofanyika hapa ni kitu muhimu sana kwetu, kwasababu wataalam wetu wanapata ujuzi mkubwa zaidi kwenye magonjwa ya damu na upatikanaji wa damu na ni heshika kwetu kama nchi kwasababu ni mara ya kwanza yanafanyika nchini kwetu,” amesema.
Aidha Makamu wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Prof Andrea Pembe amesema kuwa kwa idadi ya watoa huduma ya afya Tanzania ni chache ukilinganisha na iddi ya Watanzania wote hivyo nguvu kubwa inahitajika kuongeza watoa huduma katika vituo vya afya.
Amesema kuwa Hospitali za Kanda na Rufaa zina upungufu wa madaktari bingwa na zinahitaji takriban zaidi ya 500 ambapo ni asilimi 79.
“Serikaali kwa ujumla imekuwa ikijitahidi kutoa ufadhiri kwa watu ili waende wakasome lakini kutokana na uwezo wa kusomesha kuwa mdogo hivyo inakuwa ngumu kufanya hivyo,” amesema.
Leave a comment