Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kutaifisha mashamba ya MO Dewji
Habari Mchanganyiko

Serikali kutaifisha mashamba ya MO Dewji

Spread the love

SERIKALI imekusudia kuchukua baadhi ya mashamba yanayomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises na kuwapa wananchi kwa kuwa kampuni hiyo imeshindwa kutimiza masharti ya uendelezaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo ya serikali imekuja baada ya Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabulla kufanya ziara ya ukaguzi wa mashamba 14 yanayomilikiwa na kampuni hiyo katika wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.

Katika ziara hiyo, Waziri Mabulla alibaini kwamba Mohammed Enterprises inamiliki maeneo yenye ukubwa wa hekta 9, 418 yaliyo sawa na hekari 20,779 ambayo kampuni hiyo imechukulia mkopo kwa ajili ya kupanda mkongwe.

“Wizara yangu imejiridhisha kuwa ipo haja ya kugawa maeneo yanayomilikiwa na Mohammed Enterprises ambayo hayajaendelezwa kwa kupandwa mkonge ili wapewe wananchi ambao wana uhaba wa ardhi muda mrefu kwa sababu ya maeneo makubwa kumilikiwa na watu wachache,” amesema Waziri Mabulla.

Kwa upande wake Meneja anayesimamia mashamba hayo kutoka Mohammed Enterprises, Newalo Nyari amejitetea kwa kusema kuwa mashamba hayo waliyaendeleza na kwamba maeneo yaliyo baki waliyaacha kwa ajili ya uhifadhi wa misitu na kuwapa wananchi kwa ajili ya kupanda mazao yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!