SERIKALI imekusudia kuchukua baadhi ya mashamba yanayomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises na kuwapa wananchi kwa kuwa kampuni hiyo imeshindwa kutimiza masharti ya uendelezaji wake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Hatua hiyo ya serikali imekuja baada ya Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabulla kufanya ziara ya ukaguzi wa mashamba 14 yanayomilikiwa na kampuni hiyo katika wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.
Katika ziara hiyo, Waziri Mabulla alibaini kwamba Mohammed Enterprises inamiliki maeneo yenye ukubwa wa hekta 9, 418 yaliyo sawa na hekari 20,779 ambayo kampuni hiyo imechukulia mkopo kwa ajili ya kupanda mkongwe.
“Wizara yangu imejiridhisha kuwa ipo haja ya kugawa maeneo yanayomilikiwa na Mohammed Enterprises ambayo hayajaendelezwa kwa kupandwa mkonge ili wapewe wananchi ambao wana uhaba wa ardhi muda mrefu kwa sababu ya maeneo makubwa kumilikiwa na watu wachache,” amesema Waziri Mabulla.
Kwa upande wake Meneja anayesimamia mashamba hayo kutoka Mohammed Enterprises, Newalo Nyari amejitetea kwa kusema kuwa mashamba hayo waliyaendeleza na kwamba maeneo yaliyo baki waliyaacha kwa ajili ya uhifadhi wa misitu na kuwapa wananchi kwa ajili ya kupanda mazao yao.
Leave a comment