Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali kuinadi Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
Elimu

Serikali kuinadi Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

PROFESA Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, amesema Serikali imejipanga kuandaa na kutoa mafunzo ya uwezeshaji wa programu za kisomo na kufanya kampeni kwa kanda za kitaaluma ili watu waelewe kazi za Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Ndalichako amesema hayo wakati akizindua Bodi ya Wakurugenzi ya Taasisi hiyo ambayo baadhi ya watu wakiwemo wabunge bungeni walikuwa wakishinikiza ifutwe kufuatia kutokuwa na ufahamu wa majukumu ambayo taasisi hiyo inafanya.

“Watu wamekuwa wanauliza kuwa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inafanya nini lazima tufanye kampeni ya kisomo ili muonekane, watu wajue mnafanya nini na waweze kuja kujiunga,” amesema.

Profesa Ndalichako amesema kuwa imani yake ni kuwa Bodi hiyo mpya kwa kushirikina na Menejimenti ya Taasisi hiyo itaweza kupunguza idadi ya watu wasiojua kusoma na kuandika.

Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012 idadi ya wasiojua kusoma na kuandika imekuwa ni asilimia 22 ambayo Waziri Ndalichako amesema idadi hiyo ilikuwa kubwa hivyo ipungue.

Naye Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Naomi Katunzi amesema anamshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini kumpa nafasi hiyo na kuwa pamoja na nafasi mbalimbali alizowahi kushika katika serikali ya Tanzania lakini amebobea kwenye masuala ya mitaala hivyo kitendo cha Rais kumteua kuwa Mkurugenzi wa Bodi hiyo ambayo mitaala imezungumzwa kwa kiasi kikubwa ni kama amerudishwa nyumbani.

Amesema atahakikisha anaisimamia taasisi hiyo ipasavyo kama matakwa ya serikali ilivyotaka ili kuhakikisha idadi hiyo ya wasiojua kusoma na kuandika inapungua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!