Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ
Habari Mchanganyiko

Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ

Dk. Hassan Abbas, Katibu Mkuu wizara ya Habari
Spread the love

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo, Dk. Hassan Abbas amesema ofisi yake inafuatilia sababu ya watumishi wawili wa Kamati ya Kimataifa ya Kuwalinda Waandishi wa Habari (CPJ), kushikiliwa na kuhojiwa na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa Idara ya Uhamiaji nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dk. Abbas ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali katika ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa “Ofisi yangu inafuatilia kujua kwa nini wanaoitwa waandishi wa habari wa CPJ waliruhusiwa kuingia nchini lakini baadaye wakalazimika kuhojiwa na uhamiaji na kuachiwa.”

Watumishi hao ni Mratibu wa Programu Barani Afrika, Angela Quintal na Mwakilishi wa CPJ Kusini mwa Jangwa la Sahara, Muthoki Mumo wameachwa huru baada ya kushikiliwa na Idara ya Uhamiaji, vile vile, taarifa zinaeleza kuwa, hati zao za kusafiria pia wamerudishiwa.

Watumishi hao walikamatwa usiku wa Jumatano wakiwa kwenye hoteli ya Southern Sun na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa serikali, na kuachwa huru baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!