Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kuanzia soko huria na madini
Habari za Siasa

Serikali kuanzia soko huria na madini

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kuanzisha soko huria la madini (Tanzania Mineral Exchange) ifikapo mwezi Desemba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki wakati akihutubia kwenye kikao cha menejimenti ya wizara ya madini na taasisi zake ambapo wataalamu kutoka Kampuni ya Tanzania Mecantile Exchange PLC-TMC waliwasilisha mada juu ya elimu ya soko la bidhaa Tanzania.

“Natamani kuona ndani ya kipindi cha miezi sita vinavyoweza kufanyika vinaanza kufanyika. Lakini tutazingatia sheria, taratibu na utaalamu kuhakikisha kwamba suala hili linafanikiwa,” amesema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko alimpongeza Waziri Kairuki kwa kuanzisha wazo hilo ambalo litawezesha kuleta mageuzi katika sekta ya madini, na kuwataka wataalamu wa Wizara ya Madini kulichukulia kwa uzito suala hilo ili utekelezaji wake ufanyike kama ilivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!