Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali inaweka nguvu kwenye TEHAMA-Prof. Ndalichako
Elimu

Serikali inaweka nguvu kwenye TEHAMA-Prof. Ndalichako

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

PROFESA Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoljia amesema, serikali inatambua umuhimu wa kuwekeza katika sekta ya teknolojia ya habari na wasiliano (Tehama), ili kufikia uchumi wa viwanda ifikapo 2025. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo leo tarehe 30 Oktoba 2019, jijini Dodoma wakati akifungua Kongomano la Nne la Mtandao Jamii katika nchi za Afrika, uliofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Amesema, kwa dunia ya leo Tehama ni jambo lisilokwepeka katika kuwezesha jamii kuzifikia fursa mbalimbali.

“Mawasiliano ni nyenzo muhimu, serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili kuimarisha mawasailiano kwa wote, hadi kule ambako bado wananchi hawajafikiwa hasa vijijini,” amesema.

“Nawaombeni mtumie kongamnao hili pia katika kutathimini ukuaji wa mawasiliano nchini, baraani Afrika lakini pia dunia kwa ujumla ili kuweza kuona ni vipi tunaweza kuwafikia wale ambao bado hawajafikiwa kwa haraka,” amesema Prof. Ndalichako.

Prof. Faustne Bee, Makamu Mkuu wa UDSM amesema, mkutano huo umehusisha washiriki kutoka katika maeneo mbalimbali duniani.

Na kwamba, kongamano hilo ni la nne na Tanzania imepewa wenyeji mwaka huu ambapo washiriki kutoka Kenya, Uganda, Cameroon, Liberia, Ghana na Uhispiania wanashiriki.

Amesema, lengo la kongamano hilo ni kupeleka huduma kwa jamii kupitia mfumo wa mawimbo ya Televisheni na kuzifikia taasisi zote za serikali, zikiwemo shule katika maeneo yasiyofikiwa na huduma ya internet ifikapo 2025.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!