Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali inawasurubu askari Magereza
Habari za SiasaTangulizi

Serikali inawasurubu askari Magereza

Askari Magereza wakiwa katika maonesho jinsi wanavyomdhibiti mfungwa mkorofi
Spread the love

JOSEPH Mbilinyi ‘Sugu’ Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini (Chadema) ameing’ang’ania serikali kwenye suala la mustakabali wa mafao ya askari Magereza. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Sugu akiuliza swali la nyongeza kwa Naibu Waziri wa Fedha Dk. Ashatu Kijaji amesema kuwa askari magereza wanafanya kazi ngumu ya kulinda wahalifu lakini wanapostaafu serikali inawacheleweshea stahiki zao zaidi ya miaka miwili.

“Mheshimiwa spika, serikali inasema kuhusu askari hawa ambao wamekuwa wakisumbuliwa kutolipwa stahiki zao baada ya kustaafu wakati polisi wanaotukamata na kutupiga wanalipwa mapema lakini wahalifu wote wanarundikwa magereza kwa hiyo hawa wanakuwa na kazi ngumu,” amesema Sugu.

Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kuwa swali hilo licha ya kuwa ni refu lakini ameamua kuliacha lijibiwe kwani limeulizwa na mtu mzoefu kuliko maswali mengine yanayoulizwa kwa ubabaishaji.

Akijibu swali hilo na swali la msingi kutoka kwa mbuge wa Viti Maalum, Lucy Mlowe (Chadema), Naibu Waziri wa Fedha Dk. Ashatu Kijaji amesema Serikali inalipa mafao kwa wastaafu wote bila ya upendeleo na kuwa katika kipindi cha hivi karibuni, zililipwa jumla ya Sh 282 bilioni kwa wastaafu mbalimbali.

Naibu waziri amewaondoa hofu pia watumishi wote walioajiriwa katika miaka ya 1980 kupitia Serikali Kuu lakini wakati ule hapakuwa na makato ya mfuko wa kijamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!