Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Serengeti Boys kushuka dimbani leo, Uturuki
Michezo

Serengeti Boys kushuka dimbani leo, Uturuki

Spread the love

TIMU ya taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 Serengeti boys wanatarajia kucheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Guinea katika michuano ya UEFA assist nchini uturuki. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Timu hiyo ambayo iliondoka nchini siku ya Ijumaa imepangwa kwenye kundi A kwenye michuano hiyo sambamba na timu za Australia pamoja na wenyeji Uturuki.

Mchezo unaofuata wa Serengeti boys itakuwa Machi 6 dhidi ya Australia na kumaliza mechi ya mwisho kwenye kundi hilo dhidi ya mwenyeji Uturuki Machi 8.

Timu hiyo imekwenda kushiriki michuano hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa COSAFA 2018 nchini Botswana na kupata mwaliko wa kwenda kushiriki michuano ya UEFA assist inayoaandaliwa na shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya (UEFA).

Serengeti boys itatumia pia michuano hiyo kama sehemu ya maandalizi kuelekea kombe la mataifa afrika AFCON, kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 inayotarajiwa kufanyika nchini mwaka huu.

 

 

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!