SERIKALI imesema kuwa elimu inayostahili kutolewa nchini ni ile ambayo inajikita katika kutatua matatizo yote na ambayo ni bora na siyo bora elimu. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).
Hayo yalielezwa na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Josephat Kandege, wakati wa Ufunguzi wa kongamano la Elimu la kila Mwaka lililofanyika Jijini Dodoma.
Kongamano hilo lilijumuisha wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu, wazazi, Chama cha walimu, Maofisa wa Tamisemi, Maofisa wa Wizara ya elimu, Wakurugenzi wa halmashauri, Necta, Veta na Nacte.
Kandege alisema kuwa alisema kuwa ili kuwa na elimu bora ambayo inaweza kutatua matatizo mbalimbali ni lazima wadau wa elimu pamoja na elimu wakionyesha biidii katika utendaji kazi wao kwa manufaa ya taifa na Kizazi kijacho.
Katika kongamano hilo lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMet) kwa kushirikiana na Right to Play ambapo kauli mbinu yake ni “Ulinzi wa Mtoto ni wetu sisi wote” Kandege alisema kuwa elimu ya Tanzania inatakiwa kuboreshwa na kuwa elimu bora katika Afrika Mashariki.
Kandege alisema kuwa Serikali imeamua kuwekeza katika suala la elimu kwa Shule za serikali ili kuhakikisha kiwango cha elimu kina kuwa bora zaidi tofauti na ilivyo kuwa hapo awali.
Katika hatua nyingine Kandege alisema kuwa wanafunzi wafundishwe uhalisia wa maisha ili kufamfanya mwanafunzi aweze kuwa na ujasiri wa kujiamini na kujifunza kwa njia ya ushindani wa kuelimika kwa nchi za jirani.
Alisema iwapo elimu itaboreshwa kwa watoto wa kitanzania itasaidia watoto hao kuwa safi, kuakiri, kiuchumi na kimaadili.
Leave a comment