Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Saudi Arabia imekiri kushindwa’
Kimataifa

‘Saudi Arabia imekiri kushindwa’

Adel al-Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia
Spread the love

NAIBU Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassim amesema kuwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia inaonesha kukiri kushindwa kwake baada ya kukubali kuanzishwa maeneo ya kupunguza mivutano nchini Syria, anaandika Jovina Patrick.

Jumapili ya jana Adel al-Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia akizungumza na waandishi wa habari nchini humo ikiwa ni miaka sita ya vita na baada ya kushindwa makundi ya kigaidi kwa ajili ya kuiondoa madarakani serikali ya Damascus, alisema kuwa Saudia inakubaliana na pendekezo la kuanzishwa maeneo ya kupunguza mizozo nchini humo.

Lengo kuu la mazungumzo hayo ni kutiwa saini makubaliano yenye lengo la kuanzishwa maeneo ya kupunguza migogoro nchini Syria. Kufuatia hali hiyo Sheikh Naim Qassim akizungumza na kanali ya televisheni ya al-Manar amesema kuwa, Saudia inapitia wakati na kipindi kigumu kutokana na kushindwa mipango yake yote katika eneo la Mashariki ya Kati.

Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, muqawama nchini Syria umekuwa ukisajili ushindi na kwamba ushindi huo utaendelea

Ameongeza kuwa, kukombolewa mji wa Aleppo kumefelisha njama za maadui za kutaka kuigawa vipande nchi ya Syria na kwamba kukombolewa mji wa Deir ez-Zor, ni ushindi mwingine mkubwa dhidi ya genge la kigaidi la Daesh.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!