Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sasa naomboleza kifo cha mama – kabendera
Habari Mchanganyiko

Sasa naomboleza kifo cha mama – kabendera

Spread the love

ERICK Kabendera, mwandishi wa habari za uchunguzi ndani na nje ya nchi, amesema ‘sasa naomboleza kifo cha mama yangu.” Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Kabendera ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuachwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, tangu tarehe 5 Agosti 2019 alipokuwa akishikiliwa kwa makosa ya matatu likiwemo la utakatishaji fedha.

Mama yake Kabendera, Verdiana Mjwahuzi alifariki dunia tarehe 31 Desemba 2019 na kuzikwa tarehe 4 Januari 2020, mkoani Kagera.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 24 Agosti 2020, baada kuachiwa huru kwa kulipa faini ya Sh. 250,000 na Sh. 100 milioni baada ya kuamriwa na mahakama, Kabendera amesema atakutana na watu wachache walimfariji tangu akumbane na mkasa huo.

Pia amewashukuru wanahabari wenzake wanaharakati, watu wa kada mbalimbali na Watanzania wote kwa kuwa naye karibu wakati akiwa kwenye matatizo.

Kabendera ameondoka na ndugu zake kwenye viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi saa 10 alasiri.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

error: Content is protected !!