Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia akemea ‘vita’ ya uwekezaji
Habari za Siasa

Samia akemea ‘vita’ ya uwekezaji

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amekemea vita baina ya wawekezaji hasa wanaozalisha bidhaa zinazofanana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza kabla ya kuzindua maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na viwanda vilivyomo Mkoa wa Pwani leo tarehe 29 Oktoba 2018, Samia amesema, hakuna haja ya wawekezaji kupigana vita wenyewe kwa wenyewe bali watafute njia ya kuboresha bidhaa zao ili zipate soko.

Samia amesema, katika Mkoa wa Pwani kuna changamoto ya wawekezaji kupigana vita, ambapo ameutaka uongozi wa mkoa huo kukaa na wawekezaji ili kuondoa changamoto hiyo.

“Changamoto ni kupigana vita wawekezaji kwa wawekezaji, hasa wa bidhaa zinazofanana, uongozi wa mkoa uangalie hilo, hakuna haja wawekezaji kwa wawekezaji kupigana vita, mkuu wa mkoa hilo nakuachia wewe kwa sababu unajua uwekezaji wako,” amesema.

Katika hatua nyingine, Samia amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo kuingia makubaliano na wawekezaji wanaotumia malighafi zinazochimbwa, ili wapande miti katika mashino wanayochimba, kuepuka maeneo kuwa jangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!