Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Samatta njia panda Aston Villa
Michezo

Samatta njia panda Aston Villa

Mbwana Samatta
Spread the love

NAHODHA wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Mbwana Samatta anayekipiga kwenye klabu ya Astorn Villa huenda akauzwa katika dirisha hili kubwa la usajili kufuatia uongozi wa klabu hiyo kumsajili Ollie Watkins kutoka klabu ya Brentford. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Samatta mwenye umri wa miaka 27, alijiunga na Astorn Villa kwenye dirisha dogo la usajili mwezi Januari akitokea klabu ya Genk inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ubelgiji.

Baadhi ya vyombo vya habari kutoka nchini Uingereza vimeripoti kuwa Samatta ni moja ya wachezaji watakaondoka kwenye klabu kabla ya dirisha la usajili kufungwa 4 Oktoba, 2020 licha ya kudumu kwa miezi nane.

Taarifa zinaeleza kuwa huenda mshambuliaji huyo akatimkia kwenye klabu ya Besiktas inayoshiriki Ligi Kuu nchini Uturuki ambayo imeonesha nia ya kuhitaji huduma ya mshambuliaji huyo.

Maamuzi ya kuondoka baadhi ya nyota ndani ya klabu hiyo yamekuja baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Dean Smith kutaka kufanya marekebisho kwenye kikosi hicho kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Mpaka sasa mshambuliaji huyo amecheza jumla ya michezo 14 toka ajiunge na Astorn villa kwenye Ligi Kuu na kufunga bao moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!