Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sakata la THRDC: LHRC yaiangukia serikali ya Tanzania
Habari Mchanganyiko

Sakata la THRDC: LHRC yaiangukia serikali ya Tanzania

Flugence Massawe, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC)
Spread the love

FLUGENCE Massawe, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC), ameshauri mamlaka husika (Wizara ya Mambo ya Ndani) kutatua utata ulioibuka dhidi ya Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

“LHRC tunaamini kwamba, mamlaka husika zitalishughulikia suala hili kwa haraka, ili kuiwezesha taasisi ya THRDC kuendelea na kazi zake,” inaeleza taarifa iliyotolewa na Massawe kwa vyombo vya habari leo tarehe 19 Agosti 2020.

Aidha, LHRC imeeleza kuwa, imeshtushwa na taarifa za THRDC kusitisha shughuli zake huku ikitoa pole kwa uongozi wa mtandao huo kufuatia changamoto inazopitia wakati huu.

           Soma zaidi:-

“LHRC tumeshtushwa sana na taarifa zilizotolewa na THRDC kuhusu kusitisha shughuli zake kwa muda kufuatia kufungwa kwa akaunti za benki za taasisi hiyo.”

“Tunatoa pole kwa Bodi ya Wakuruenzi mratibu na wanachama kwa usumbufu wanaoupitia,” imeeleza taarifa ya LHRC.

THRDC uliitangazia umma wa Tanzania tarehe 17 Agosti 2020 kwamba unasitisha shughuli zake, baada ya kukumbwa na changamoto za kifedha za uendeshaji, kufuatia akaunti yake katika Benki ya CRDB kufungwa na Jeshi la Polisi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vicky Ntetema, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya THRDC , Jeshi la Polisi limefunga akaunti hiyo, ili kufanyia kazi masuala yaliyoko mbele yake.

Hata hivyo, taarifa hiyo inaeleza kwamba, Onesmo Ole Ngurumwa, Mratibu wa THRDC siku ya Jumatatu alihojiwa na Jeshi la Polisi kuhusu tuhuma zinazo kabili mtandao huo, za kutowasilisha mikataba yake na wafadhili katika Ofisi ya Hazina na Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!