Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sakata la ‘Bashite’ kutolewa maelezo kesho
Habari Mchanganyiko

Sakata la ‘Bashite’ kutolewa maelezo kesho

Spread the love

TUME  ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inatarajia kumhoji Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob kuhusu  madai yake aliyowasilisha kwa tume hiyo akitaka Mkuu wa  Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwamba ameghushi vyeti vya shule, anaandika Faki Sosi.

Jacob amesema kuwa tume hiyo imemtaka afike ofisini kwao kesho asubuhi ili aweze kutoa maelezo juu ya mashtaka yake juu ya Makonda.

Meya huyo ambaye pia ni Diwani wa Ubungo amesema ameitwa kupitia barua yenye kumbukumbu namba  CAG 31/37/01/42.

Hata hivyo, Jacob amesema kuwa tayari kuna viashiria vya vishawishi vya yeye kuachana na shauri hilo linalomkabili Makonda.

Mwezi Machi mwaka huu  Jacob aliwasilisha mashtaka manne katika tume hiyo pamoja na moja la  jinai ambalo ni la kughushi  vyeti vya taaluma.

Hivi karibuni Makonda alipachikwa jina la Bashite ambalo linadaiwa ndilo jina lake halisi alilopewa na wazazi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!