Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sadaka misa ya Mkapa kukarabati nyumba ya mapadri Lupaso
Habari Mchanganyiko

Sadaka misa ya Mkapa kukarabati nyumba ya mapadri Lupaso

Marehemu Benjamin Mkapa
Spread the love

YUDA Rua’ichi, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam ameagiza, sadaka itakayopatikana kwenye shughuli ya kumuaga Benjamin William Mkapa, Rais mstaafu wa awamu ya tatu zitumike kukarabati nyumba ya mapadri ya Lupaso, Mtwara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetangazwa leo tarehe 26 Julai 2020, kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam ambapo sala na shughuli ya kuaga mwili wa Mzee Mkapa aliyefariki dunia Alhamisi tarehe 23 Julai 2020, zikiendelea.

“Mzee Mkapa alikuwa na nia ya kukarabati nyumba ya mapadri ya parokia ya Lupaso, ukarabati huo unakadiriwa kutumia si chini ya Sh. 20 milioni. Hiyo nyumba tangu ilipojengwa na wale wamisionari wa kwanza, haijafanyiwa ukarabati.”

“Mhashama Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Rua’ichi kwa niaba ya Baraza la Maaskofu Tanzania, ameagiza sadaka hii ya leo itakuwa ni kwa ajili ya kumuenzi mzee wetu kwa ukarabati wa nyumba hiyo,” imeeleza taarifa hiyo.

Misa ya kumuaga mwili wa Rais Benjamin Mkapa

Shuhuli ya kuaga mwili wa Mzee Mkapa itafanywa kwa siku tatu kuanzia leo hadi Jumanne tarehe 28 Julai 2020 na kisha, atapelekwa kuzikwa kijijini kwake Lupaso, Mtwara Jumatano tarehe 29 Julai 2020.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!