Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Sababu ongezeko vifo ajali ya Lori Morogoro yaelezwa
Afya

Sababu ongezeko vifo ajali ya Lori Morogoro yaelezwa

Spread the love

HATUA ya majeruhi wengi wa ajali ya Lori la mafuta lililowaka moto Morogoro, walifikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimibi (MNH) kuendelea kupoteza maisha, ni kutokana na kuungua kwa asilimia 80 hadi 90. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Mpaka sasa majeruhi 32 kati ya 47 walifikishwa MNH, wamefariki dunia ambapo waliobaki 15 wote wako kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).

Ufafanuzi huo umetolewa leo tarehe 21 Agosti 2019 na Dk. Laurian Rwanyuma, daktari bingwa wa upasuaji katika hospitali hiyo, na kwamba majeruhi wengi waliungua sehemu za ndani ikiwemo mfumo wa hewa na figo.

“Kuungua kwa ndani kumesababisha kupumua kwao kuwa kwa shida,.. kutokana na ngozi zao kuungua kwa asilimia kubwa, hali hiyo imesababisha mwili kukosa kinga na kupoteza maji mengi,” amesema Dk. Rwanyuma na kuongeza;

“Kwa kawaida wagonjwa walioungua kiasi hicho, wana uwezekano mdogo wa kupona hata kama hospitali ina uwezo mkubwa wa vifaa na dawa.”

Dk. Rwanyuma amewaeleza wanahabari kwamba, madaktari wanaendelea kufanya juhudi zao kuhakikisha majeruhi waliobaki wanapata afueni na kupona.

Mpaka sasa, tayari watu 100 katika ajali hiyo ilitokea tarehe 10 Agosti 2019, Morogoro wamefariki.

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!