MKURUGENZI wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amefariki dunia leo nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Awali, taarifa za kifo cha Ruge zilianza kujulikana mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kuandika kupitia ukurasa wake wa mtandao wa twitter kuwa amepata taarifa ya kifo hicho.
“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha kijana wangu Ruge Mutahaba. Daima nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk tasnia ya habari, burudani, na juhudi za kujenga fikra za maendeleo kwa vijana. Poleni wanafamilia,ndugu,jamaa na marafiki. Mungu amweke mahali pema, Amina,” aliandika Rais Magufuli kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.
Hadi umauti unamfika, Ruge alikuwa nchini Afrika Kusini akipatiwa matibabu ambapo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Figo, aliugua kwa zaidi ya miezi minne akaanza kupatiwa matibu Dar es Salaam katika hospitali ya Kairuki, akapelekwa India na baadae Afrika Kusini ambapo ndipo umauti ulipomkuta.
MwanaHALISI ONLINE itakujuza zaidi. Pumzika kwa amani Ruge Mutahaba.
Leave a comment