Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ruge Mutahaba afariki dunia, Rais Magufuli amlilia
Habari MchanganyikoTangulizi

Ruge Mutahaba afariki dunia, Rais Magufuli amlilia

Spread the love

MKURUGENZI wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amefariki dunia leo nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Awali, taarifa za kifo cha Ruge zilianza kujulikana mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kuandika kupitia ukurasa wake wa mtandao wa twitter kuwa amepata taarifa ya kifo hicho.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha kijana wangu Ruge Mutahaba. Daima nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk tasnia ya habari, burudani, na juhudi za kujenga fikra za maendeleo kwa vijana. Poleni wanafamilia,ndugu,jamaa na marafiki. Mungu amweke mahali pema, Amina,” aliandika Rais Magufuli kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.

Hadi umauti unamfika, Ruge alikuwa nchini Afrika Kusini akipatiwa matibabu ambapo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Figo, aliugua kwa zaidi ya miezi minne akaanza kupatiwa matibu Dar es Salaam katika hospitali ya Kairuki, akapelekwa India na baadae Afrika Kusini ambapo ndipo umauti ulipomkuta.

MwanaHALISI ONLINE itakujuza zaidi. Pumzika kwa amani Ruge Mutahaba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!