Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mwanri: Naomba radhi
Habari za Siasa

RC Mwanri: Naomba radhi

Agrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora
Spread the love

AGREY Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa mwanzoni mwa mwezi Aprili 2019 kwamba, Mungu amshukuru Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya za kuliletea maendeleo taifa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mkoani Tabora, Mwanri amesema, hakuna binadamu anayeweza kuchukua nafasi ya Mungu huku akisistiza kwamba, atakua amechuja sana endapo ataamini hilo.

Mwanri amefafanua kuwa, kauli yake haikuwa na maana mbaya bali ilitafsiriwa tofauti na baadhi ya watu.

Amesema, dhamira yake ilikua ni kutaka kuona kwamba Mwenyezi Mungu anamshukuru Rais Magufuli kutokana na mema anayofanya ya kutetea masilahi ya wangine.

“Ila nilichojifunza ni kwamba, inapopelekwa habari inapokelewa na masikio mengi usifikiri hata kama uko sawa itapokelewa hivyo hivyo, bali itapokelewa tofauti.

“Sina cha zaidi ya kuomba msamaha kwa sababu nimeshafafanua na mimi walioninukuu vibaya natangaza kuwasemehe,” amesema Mwanri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!