Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa
Habari Mchanganyiko

RC Mbeya sasa kuchapa viboko wasiofunga ndoa

Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

ALBERT Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ametangaza kuwachapa bakora wanaume na wanawake wasiofunga ndoa. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Chalamila ametangaza kampeni hiyo kufuatia mijadala iliyoibuka mitandaoni hivi karibuni, juu ya changamoto ya wanawake wengi kutoolewa, ambapo baadhi ya wananchi wakinyooshea vidole wanaume kwamba wamekuwa wagumu kuoa.

Mkuu huyo wa wilaya ameeleza, mwanamke atakayekutwa hajaolewa, na mwanaume atakayekutwa hajaoa, atatatindwa bakora ili akatafute mume au mke.

“Maana siku hizi tunaanza kutumia viboko katika kila jambo, hata tukikuta umekaa pale nyumbani huolewi ni bakora tu, nenda katafute mume.

“Tunakuona umekee pale nyumbani huoi ni bakora tu nenda katatufute mke. Kuna umri ambao unatosha lazima uchangamshwe kwa hiyo viboko vinasaidia,” amesema Chalamila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!