Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Kunenge atangaza fursa za biashara Dar
Habari za Siasa

RC Kunenge atangaza fursa za biashara Dar

Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Aboubakar Kunenge amewataka wafanyabishara kuchangamkia fursa ya baishara katika Kituo cha Kimataifa cha Mabasi Mbezi Lius jijini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kituo hicho kitakachokuwa kikuhudumia mabasi ya mikoani na yanayokwenda nje ya mipata ya Tanzania, ujenzi wake umefikia asilimia 90.

RC Kunenge amesema hayo leo Jumatatu tarehe 9 Novemba 2020 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema, majaribio ya kituo hicho itakuwa tarehe 25 Novemba 2020 na kutumika rasmi 30 Novemba.

Mkuu huyo wa mkoa, ametoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuchangamkia fursa zinazopatikana kwenye kituo hicho ikiwemo fremu za maduka, migahawa, ofisi, huduma za kifedha, supermarket, ofisi za kukata tiketi na hotel.

Kunenge amewataka wananchi wanaohitaji maeneo kutuma maombi kuanzia leo Jumatatu hadi tarehe 25 Novemba 2020.

Amesema, uwepo wa kituo hicho kitaendelea kufungua fursa za maendeleo kwa wakazi wa Ubungo hivyo amewataka kujiandaa kwa hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!