Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ratiba ya Msiba wa Dk. Mengi kesho, Makonda, Rungwe watoa neno
Habari Mchanganyiko

Ratiba ya Msiba wa Dk. Mengi kesho, Makonda, Rungwe watoa neno

Spread the love

RATIBA ya Msiba wa Reginald Mengi, Mkurugenzi wa Kampuni  za IPP zitafahamika kesho saa saba mchana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari nyumbani kwa marehemu, Michael Ngalu,  Mwanasheria na Msemaji wa Familia hiyo amesema kuwa kesho saa 7 mchana familia itatoa ratiba ya mazishi ya msiba huo.

Wakati huohuo wanasiasa kadhaa walifika kwenye msiba huo na kueleza namna walivyoguswa na msiba huo.

Hashimu Rungwe, Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), amesema kuwa msiba wa Dk. Mengi umeligusa taifa na kwamba marehemu alikuwa rafiki wa kila mtu.

Amesema kuwa kwa upande wake hakumuona Dk. Mengi akiwa mbaguzi wa kisiasa wala dini alisaidia watu wote.

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa  wa Dar es Salaam amesema kuwa taifa limepata pigo kufuatia msiba wa Dk. Mengi ambapo amekuwa na mchango kwa watu wengi nchini.

https://www.youtube.com/watch?v=pOGuHpTAw88

Amesema kuwa yeye na vijana wengine wengi walishikwa mkono na Dk. Mengi kwenye mchango wa kielimu na hata kifedha.

Amewatia moyo walemavu kuwa Mungu aliyemchukua Dk. Mengi atamleta mwingine atakayekamilisha lile aliloadhimia la kuwajengea kiwanda walemavu.

Abdallah Ambua, Mtangazaji wa East Afrika  Radio na Televisheni, amesema kuwa msiba huo ni mkubwa licha ya marehemu kuacha alama muhimu nchini kwa kuwafungulia milango ya fursa vijana, walemavu na wazee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!