Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa
Habari Mchanganyiko

Ratiba kuapishwa rais mpya Burundi yabadilishwa

Evariste Ndayishimiye, Rais wa Burundi
Spread the love

EVARISTE Ndayishimiye, rais mteule wa Burundi anatarajiwa kuapishwa kesho tarehe 18 Juni 2020, badala ya Agosti kama ilivyopangwa. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Tume ya Uchaguzi ya Burundi wakati wa mchakato wa uchaguzi, ilileleza kwamba rais atakayechaguliwa na wananchi, ataabishwa Agosti, ratiba hiyo imebadilishwa baada ya kicho cha ghafla cha rais wa taifa hilo, Pierre Nkurunziza.

Imeelezwa, Ndayishimiye angeweza kuapishwa iwapo Nkurunziza angekuwa hai, lakini sasa nchi haina rais na si busara kusubiri wakati huo wakati hakuna kikwazo chochote kwa sasa.

Ndayishimiye anayetokana na chama tawala wa CNDD-FDD, ataapishwa katika Mji wa Gitega ikiwa ni wiki moja baada ya mtangulizi wake kufariki dunia kwa mshtuko wa moyo.

Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 Juni 2020. Baada ya kuapishwa, Ndayishimiye atahudumia taifa hilo kwa kipindi cha miaka saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!