MKUFUNZI wa zamani wa Leicester City, Claudio Ranieri ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa klabu ya Fulham inayoshiriki Ligi Kuu ya England mara baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wao Slavisa Jokanovic, kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Ranieri amesema kuwa ni heshima kukubali mwaliko wa mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan na nafasi ya kuiongoza Fulham ambayo ni klabu kubwa kihistoria.
“Malengo makubwa ya Fulham hayapaswi kuishia katika ligi kuu nchini England,” alisema Ranieri.
Ikumbukwe Ranieri ndiyo kocha pekee aliyeiongoza Lecester City kutwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu England katika msimu wa mwaka 2016, akiwa na kikosi ambacho hakikughalimu kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajiri.
Fulham ambayo kwa sasa inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya kupoteza michezo tisa kati ya 12 waliocheza na kuruhusu mabao 31, licha ya mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajili.
Leave a comment