Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Ranieri kumrithi Jokanovic Fulham
Michezo

Ranieri kumrithi Jokanovic Fulham

Claudio Ranieri
Spread the love

MKUFUNZI wa zamani wa Leicester City, Claudio Ranieri ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa klabu ya Fulham inayoshiriki Ligi Kuu ya England mara baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wao Slavisa Jokanovic, kutokana na matokeo mabovu ya timu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Ranieri amesema kuwa ni heshima kukubali mwaliko wa mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan na nafasi ya kuiongoza Fulham ambayo ni klabu kubwa kihistoria.

“Malengo makubwa ya Fulham hayapaswi kuishia katika ligi kuu nchini England,” alisema Ranieri.

Ikumbukwe Ranieri ndiyo kocha pekee aliyeiongoza Lecester City kutwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu England katika msimu wa mwaka 2016, akiwa na kikosi ambacho hakikughalimu kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajiri.

Fulham ambayo kwa sasa inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya kupoteza michezo tisa kati ya 12 waliocheza na kuruhusu mabao 31, licha ya mmiliki wa klabu hiyo Shahid Khan kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye usajili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!