NAHODHA wa Real Madrid, Sergio Ramos anaonekana kutokukubaliana na ujio wa kocha wa zamani wa Chelsea Antonio Conte ndani ya kikosi hicho baada ya kutimuliwa Julen Lopetegui kufuatia kuwa na matokeo mabaya kwenye michezo ya ligi kuu nchini humo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Nahodha huyo anaonekana kutofurahishwa na aina ya uwendeshaji timu wa Conte, kutokana na kuingia mara kwa mara kwenye migogoro na wachezaji.
Hali hiyo inakuja baada ya Conte kuwa katika moja ya makocha wanaopendekezwa kwenda kuchukua mikoba ya Lopetegui ambaye alitimuliwa jana baada ya kupoteza mchezo kwa bao 5-1 dhidi ya Barcelona siku ya Jumapili na timu hiyo kwa sasa ipo chini ya Santiago Solar kwa muda.
Conte ambaye alitimuliwa kwenye klabu ya Chelsea mwisho wa msimu uliopita baada ya kuwa katika matatizo na baadhi ya wachezaji wa klabu hiyo akiwemo Eden Hazard ambaye huwenda akahamia Madrid katika majira ya joto.
Kwenda kwake Madrid huwenda kukakwamisha uhamisho Hazard kutoka Chelsea kutokana ya kutokuwa na maelewano mazuri baina ya wawili hao hapo awali.
Matatizo hayo binafsi kati ya Conte na baadhi ya wachezaji wa Chelsea yalipelekea timu hiyo kushika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi na hivyo kushindwa kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya katika msimu huu.
Leave a comment