Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais wa Burundi atua Kigoma, JPM ampokea
Habari za Siasa

Rais wa Burundi atua Kigoma, JPM ampokea

Spread the love

EVARISTE Ndayishimiye, Rais wa Burundi amewasili mkoani Kigoma nchini Tanzania katika ziara ya kiserikali ya siku moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Rais Ndayishimiye amewasili mkoani humo leo Jumamosi tarehe 19 Septemba 2020 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Kiongozi huyo wa Burundi amefanya ziara ya kwanza tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Taifa hilo Mei 2020.

Katika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma, Rais Magufuli amempokea Rais Ndayishimiye ambapo zimepigwa nyimbo za mataifa hayo mawili na ule wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kukagua gwaride maalum.

 

Rais huyo wa Burundi amewasili nchini Tanzania baada ya kualikwa na Rais Magufuli.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Taifa, Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza uwanjani hapo amempongeza Rais Ndayishimiye kwa kuchagua Tanzania kuwa nchi ya kwanza kutembelea tangu achaguliwe.

Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online, MwanaHalisi TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!