Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump kupandishwa kizimbani
Kimataifa

Rais Trump kupandishwa kizimbani

Spread the love

RAIS wa Marekani, Donald Trump ameshtakiwa katika mahakama ya wilaya ya Kaskazini iliyoko kwenye jimbo la Calfornia, kwa kutangaza hali ya dharura ili akusanye fedha za ujenzi wa ukuta ulioko mpakani mwa taifa hilo na nchi ya Mexico. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kesi hiyo imewasilishwa jana Jumatatu katika mahakama ya wilaya ya Kaskazini na muungano wa majimbo 16 ya nchini Marekani, yakiongoza na jimbo la Calfornia, ukiwa na lengo la kuiomba mahakama kuzuia matumizi mabaya ya nguvu za rais.

Mkuu wa Sheria katika jimbo la California, Xavier Becerra amedai kuwa, wanamshtaki Rais Trump ili kumzuia kutumia vibaya pesa za walipa kodi wa Marekani zilizotengwa kisheria na bunge kwa ajili ya matumizi ya watu walioko katika majimbo hayo 16.

Katika kesi hiyo, muungano huo umeiomba mahakama kutoa zuio kwa Rais Trump kutotekeleza mpango wake wa ujenzi wa ukuta hadi pale kesi itakapoanza kusikilizwa na kutolewa maamuzi.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Rais Trump akiwa Ikulu ya ‘White House’ alitangaza hali ya hatari ili apate fursa ya kukusanya dola 8 bilioni kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa ukuta huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!