Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump atishia kuangamiza vyombo vya habari
Kimataifa

Rais Trump atishia kuangamiza vyombo vya habari

Spread the love

RAIS Donald Trump ametangaza vita na vyombo vya habari nchini mwake kwa madai kwamba vimekuwa vikikiuka taratibu na kuonyessha ama kuandika habari kwa upendeleo, anaandika Mwandishi Wetu.

Amesema anaweza kufuta leseni za vituo vya runinga nchini mwake kutokana na kuwapo na kasoro za ukiukwaji wa tararibu.

Moja ya vitu vilivyomkasirisha Rais Trump ni pamoja na kituo cha runinga cha NBC kutangaza habari kwamba yeye aliwaagiza maofisa wake wa usalama pamoja na majenerali kuongeza kiwango kikubwa cha silaha za kinyuklia nchini humo.

Rais huyo alisema kuwa habari hiyo ilitungwa huku waziri wake wa ulinzi, Jim Mattis akisema taarifa hiyo haikuwa na ukweli wowote.

Wiki iliopita kituo cha NBC kilitoa taarifa kwamba waziri wa masuala ya kigeni nchini Marekani, Rex Tillerson alimuita Trump ‘mtu mjinga’ matamshi ambayo hayajakanushwa lakini ambayo rais huyo ameyataja kuwa habari bandia.

Wanahabari wanasema kuwa rais huyo atapata shida kufuta lesen za vyonbo vya habari. Leseni za vyombo vya habari zinadhibitiwa na tume ya mawasiliano nchini humo.

Baadhi ya makundi ya kupigania haki yanasema kuwa rais Trump anaweka mfano mbaya kwa viongozi wengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!