Donald Trump, Rais wa Marekani anachunguzuwa na Robert Mueller, ambaye ni mwanasheria maalum kwa kile kinachotajwa kuwa alizuia sheria, kwa mujibu wa gazeti la Washington Post.
Gazeti hilo linaeleza kuwa maafisa watatu wa vyeo vya juu wamekubali kuhojiwa na wachunguzi wa Mueller.
Wakili wa Trump walisema kuwa hatua ya FBI kifichua taarifa kwa gazeti hilo ni kitendo kibaya.
Muller anaongoza uchunguzi wa FBI kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani mwaka 2016 na uhusiano wowote wa Trump kwa suala hilo.
Rais Trump mara kwa mara amekuwa akikana kuwa na ushirikiano wowote na Urusi.
Siku ya Jumatano gazeti la washington post lilitaja hatua ya Muller kuchunguza mienendo ya Rais Trump kama hatua kubwa katika uchunguzi huo.
Maafisa ambao hawakutajwa walieleza gazeti hilo kuwa uchunguzi kuhusu Trump kuzuia sheria ulianza siku kadha baada ya Trump kumfuta mkuu wa FBI James Comey tarehe 9 mwezi Mei.
Kabla hajafutwa kzi, Trump alikuwa amepewa hakikisho kutoka kwa Comey kuwa sio yeye alikuwa akichunguzwa.
Hata hivyo Comey tangu wakati huo amedai kuwa Trump amejitahidi kumshawishi aachane na uchunguzi dhidi ya mshauri wake wa masuala ya usalama Machael Flynn.
Flynn alifutwa mwezi Februari kwa kushindwa kufichua kiwango cha uhusiano wake na Sergei Kislyak, ambaye ni balozi wa Urusi nchini Marekani.
Leave a comment