ROBERT Mugabe, aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zimbabwe, amefariki dunia. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Taarifa kutoka ndani ya familia ya gwiji huyo wa siasa, ambaye alikuwa mpigania uhuru wa nchi hiyo zimeeleza, kiongozi huyo amefariki dunia nchini Singapore baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Rais Mugabe alipigania uhuru wa Zimbabwe ambayo ilipata uhuru tarehe 18 Aprili 1980.
Aliliongoza taifa hilo kwa takriban miongo mitatu, hadi alipoondolewa madarakani kwa njia ya mapinduzi ya kijeshi Novemba 2017.
Aliyechukua nafasi yake ni aliyekuwa makamu wake wa rais, Emmerson Mnangagwa na baadaye wa rais, badadaye alichaguliwa kuwa rais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2019.
Fadzayi Mahere, Waziri wa Elimu wa Zimbabwe, ametoa taarifa ya kifo cha Mugabe kupitia ukurasa wake wa Twitter akiandika “Pumzika kwa amani Robert Mugabe.”
Robert Mugabe pia aliwahi kufungwa jela kwa zaidi ya muongo mmoja bila kufunguliwa kesi, ni baada ya kuikosoa Serikali ya Rhodesia mwaka 1964.
Naye Rais Mnangagwa ameandika kupitia ukurasa wake wa twitter kuhusu kifo cha Mugabe na kusema kuwa, mchango wake hautasaulika.
“Mchango wake katika historia ya Taifa letu kamwe hautasaulika. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele,”amesema.
Rais Mugabe alizaliwa Februari 21, mwaka 1924 katika nchi hiyo wakati huo ikiitwa Rhodesia na ameacha mke ambaye ni Grace Mugabe na watoto wanne ambo ni Bona Mugabe, Chatunga Bellarmine Mugabe, Robert Peter Mugabe Jr., Michael Nhamodzenyika Mugabe.
Leave a comment