Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Mwinyi kutangza mawaziri kesho
Habari Mchanganyiko

Rais Mwinyi kutangza mawaziri kesho

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi kesho Alhamisi tarehe 19 Novemba 2020, ataweka wazi sura ya baraza lake jipya la mawaziri. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, atakuwa anaunda baraza hilo la kwanza tangu alipoingia madarakani tarehe 2 Novemba 2020.

Rais Mwinyi aliingia madarakani akichukua nafasi ya mtangulizi wake, Dk. Ali Homahed Shein aliyemaliza miaka kumi ya utawala wake kwa mujibu wa Katiba.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano na Hassan Hassan, Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na Habari, Ikulu imesema, Rais Mwinyi atatangaza baraza hilo, kesho Alhamisi saa 4:00 asubuhi

Taarifa hiyo ya uteuzi, imezidisha presha kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuona nani atateuliwa ili kuanza safari ya miaka mitano ya kuwatumikia Wazanzibar kwenye nafasi watakazoteuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!