RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewasili Uwanja wa Ndege wa Chato Mkoa wa Geita na kupokewa na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli ili kushuhudia utiaji saini mkataba ujenzi mradi wa bomba la mafuta. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).
Shughuli hiyo inafanyikia Uwanja wa Ndege wa Chato huku kukiwa na tahadhari zote za kujikinga na maambukizo ya virusi vya corona (COVID-19).
Viongozi mbalimbali wa kiserikali kama mawaziri na watebdaji wa taasisi na wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanashiriki shughuli.
Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online na MwanaHalisi TV kwa habari zaidi.
Leave a comment