Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Mnangawa achekelea Uchaguzi Zimbabwe
Kimataifa

Rais Mnangawa achekelea Uchaguzi Zimbabwe

Spread the love

WAKATI kura zikiendelea kuhesabiwa katika uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika, Rais wa nchi hiyo Emmerson Mnangawa ambaye ni mmoja wa wagombea ameonesha kuwa, ana matumaini makubwa ya kushinda baada ya kuonesha hisia zake kwenye ukurasa wake wa twitter.

Ujumbe huo unaelezea furaha yake baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wawakilishi wake waliopo kwenye vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo amesema, yeye na wafuasi wake watasubiri mpaka matokeo rasmi yatangazwe kama ilivyo taratibu za sheria za nchi hiyo.

” Good morning Zimbabwe. I am delighted by the high turnout and citizen engagement so far. The information from our reps on the ground is extremely positive! Waiting patiently for official results as per the constitution”

Rais Mnangagwa alichukua mamlaka baada ya urais baada ya jeshi kuingilia kati mnamo Novemba 15 mwaka jana kufuatia mgogoro wa kumrithi mhasisi wa nchi hiyo Robert Mugabe.

Huku matokeo ya awali yakitarajiwa kutangazwa muda wote kuanzia sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!