WAKATI kura zikiendelea kuhesabiwa katika uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika, Rais wa nchi hiyo Emmerson Mnangawa ambaye ni mmoja wa wagombea ameonesha kuwa, ana matumaini makubwa ya kushinda baada ya kuonesha hisia zake kwenye ukurasa wake wa twitter.
Ujumbe huo unaelezea furaha yake baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wawakilishi wake waliopo kwenye vituo vya kupigia kura.
Hata hivyo amesema, yeye na wafuasi wake watasubiri mpaka matokeo rasmi yatangazwe kama ilivyo taratibu za sheria za nchi hiyo.
” Good morning Zimbabwe. I am delighted by the high turnout and citizen engagement so far. The information from our reps on the ground is extremely positive! Waiting patiently for official results as per the constitution”
Good morning Zimbabwe. I am delighted by the high turnout and citizen engagement so far. The information from our reps on the ground is extremely positive! Waiting patiently for official results as per the constitution.
— President of Zimbabwe (@edmnangagwa) July 31, 2018
Rais Mnangagwa alichukua mamlaka baada ya urais baada ya jeshi kuingilia kati mnamo Novemba 15 mwaka jana kufuatia mgogoro wa kumrithi mhasisi wa nchi hiyo Robert Mugabe.
Huku matokeo ya awali yakitarajiwa kutangazwa muda wote kuanzia sasa.
Leave a comment