Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Uchaguzi Mkuu palepale

John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

LICHA ya kuwepo kwa tishio la kusambaa kwa virusi vya corona (COVID-19) nchini, uchaguzi mkuu unaoratajiwa kuwanyika Oktoba mwaka huu, hautaahirishwa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza jijini Dodoma leo tarehe 26 Machi 2020, Rais John Magufuli amesema, uchaguzi huo hautasogweza mbele, kwa kuwa hakuna mtu anayetaka kuendelea kukaa madarakani.

Ametoa kauli hiyo huku kukiwa na taarifa zisizothibitishwa kwamba, uchaguzi huo utafanyika mwaka 2021 kutokana na tishio la ugonjwa corona.

“Hatujazuiliwa kukutana, sisi tunaendelea kukutana na tunakutana katika mikutano ya kawaida, na uchaguzi tutafanya tu, wako wengine wanafikiri nitaahirisha, nani anataka kukaa kwenye maofisi muda wote huo?” amehoji Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema, kazi zitaendelea kufanyika ikiwemo vikao vya bunge vitaendelea.

“Hatujazuiliwa kukutana, leo nilikuwa nasoma gazeti moja linasema Madiwani wafanya kikao sijui alifikiri wamezuiliwa kukutana kwa sababu ya Corona? Sisi tunaendelea kukutana, hata nchi zilizoathirika, bado mabunge na mabaraza hayajafungwa,”amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!