RAIS John Magufuli amesema, atamkaba Waziri wa Ardhi, William Lukuvi ili amlipe Sh. 1 milioni fedha alizowapa wazee wawili ambao mmoja wao alidhulumiwa eneo lake. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 5 Septemba, 2018 wakati akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara, baada ya kupokea malalamiko ya kuporwa ardhi yaliyotolewa na wazee hayo.
Bibi Nyasasi Masige (mwenye kiwanja) akiwa na jirani yake wamemlalamikia Rais Magufuli kuwa, kuna tajiri aliyedhulimu kiwanja cha mmoja wao baada ya kumuuzia kiwanja cha pili kwa ajili ya kupata fedha za matibabu, na kwamba aliporudi kutoka kupata matibabu alikuta tajiri huyo amejimilikisha kiwanja cha pili.
Wazee hao walidai kuwa, mgogoro wao ulimfikia Waziri Lukuvi ambapo aliagiza bibi huyo kupatiwa kiwanja chake jambo ambalo halijafanyika hadi leo.
Kufuatia malalamiko hayo, Rais Magufuli alimtafuta Waziri Lukuvi kwa njia ya simu, na kumuagiza kumsimamisha kazi kamishna wa ardhi wa kanda hiyo kuanzia leo.
Baada ya hapo Rais Magufuli aliwakabidhi wazee hao kila mmoja Sh. 500,000 kutokana na usumbufu walioupata na kwamba, fedha hizo zitalipwa na Waziri Lukuvi. Rais Magufuli yupo mkoani Mara kwa ziara ya kikazi.
Leave a comment