Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Rais Magufuli: Mkifungwa watasema nimewapa mkosi
Michezo

Rais Magufuli: Mkifungwa watasema nimewapa mkosi

Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka wachezaji wa Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kuifunga timu ya taifa ya Lesotho katika mchezo wa kuwania kufuzu kucheza michuano ya mataifa ya Afrika (AFCON) 2019 nchini Cameroon, unaotarajiwa kupigwa Novemba 18 2018. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).   

Akizungumza na uongozi na wachezaji wa Taifa Stars  leo tarehe 19 Oktoba 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema timu hiyo ikifungwa itakuwa aibu na atajuta kuwaona kwa kuwa watu watasema amewapa mkosi.

“Lesotho mkifungwa itakuwa aibu nitajuta hata kuwaona, sababu mkifungwa watasema Magufuli amewapa mkosi wameenda kufungwa, vijana niwaombe msiende kufungwa. Tukiamua tutawapiga magoli mengi mno na wakija tuliocheza nao tutawatandika,” amesema Rais Magufuli.

Taifa Stars inatarajia kuifuata Lesotho tarehe 18 Novemba mwaka huu, ambapo inatakiwa kupata matokeo mazuri ili kujihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwakani nchini Cameroon.

Hadi sasa Taifa Stars iko nyuma ya Uganda kwa kushika nafasi ya pili katika kundi L, baada ya kufikisha pointi tano kufuatia matokeo ya bao 2-0 iliyopata  dhidi ya Cape Verde kwenye mechi ya marudiano iliyochezwa Oktoba 16 2018 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!