Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Magufuli: Jeshi msikubali vikwazo
HabariHabari Mchanganyiko

Rais Magufuli: Jeshi msikubali vikwazo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli, Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi, ameyataka majeshi nchini kutokubali kuwekewa vikwazo, katika utekelezaji wa majukumu yake. Anaripoti Martin Kamote…(endelea)

Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 25 Novemba 2019 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo, Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma.

“Milima yote chukueni ili  mlinde vizuri nchi hii, najua mtaitumia vizuri sababu majeshi ya Tanzania ni imara, msipate vikwazo. Mtu akikaa kule na ng’ombe amewapa vikwazo. Na jeshi halitakiwi kupewa vikwazo, labda vikwazo wakati wa mazoezi, vinavyowafanya kuwa imara, “ amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amesisitiza usalama wa viongozi wa jeshi, na kuwashauri makazi yao yasijulikane hovyo.

“Lazima muelewe vitu vingine lazima viwe vyenu, kama ni nyumba anakaa CDF wengine wasipajue, kama ni nyumba anakaa askari wa jeshi wengine si lazima wapajue.

Ninatambua yale yote mliyokuwa mnayaonesha leo, ni mfano wa mtakayoyafanya sio uhalisia,” ameshauri Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!