Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awatakia Watanzania Heri ya Krismas
Habari za Siasa

Rais Magufuli awatakia Watanzania Heri ya Krismas

Rais John Magufuli
Spread the love
RAIS wa Tanzania, Dk. John Magufuli ameungana na Watanzania kuadhimisha siku ya kuzaliwa Yesu Kristo, kwa kusali Misa Takatifu ya Krismasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Misa hiyo imefanyika leo Ijumaa tarehe 25 Desemba 2020, katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Imakulata,  Chamwino mkoani Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya Gerson Msigwa, Mawasiliano ya Rais, misa hiyo iliongozwa na Paroko wa Parokia hiyo Padre Paul Mapalala.

“Rais Magufuli amewapongeza na kuwatakia heri Watanzania wote kwa sikukuu ya Krismasi na amewataka kuendelea kumshukuru Mungu kwa miujiza na upendo mkubwa anaolitendea Taifa la Tanzania,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Katika misa hiyo, Rais Magufuli amesema upendo na miujiza ya Mungu kwa Tanzania, inajidhihirisha katika kipindi hiki ambapo Dunia inapita katika wakati mgumu wa janga la ugonjwa wa Korona (Covid-19).

Ambapo maelfu ya watu wanaendelea kupoteza maisha kila siku, lakini Tanzania imeepushwa na janga hilo na maisha ya Watanzania yanaendelea kama kawaida.

Rais Magufuli ametoa wito kwa viongozi wa Mataifa mbalimbali duniani, kumweka Mungu mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Korona, badala ya kutegemea nguvu za binadamu pekee.

1 Comment

  • Vatikani kuna Corona pamoja na Mecca na Madina na Israel
    Sasa wao wamekosea wapi? Hawakumuweka Mungu mbele?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!