Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli awapa pole Waislam
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli awapa pole Waislam

Spread the love

RAIS John Magufuli ametuma pole kwa Waislam nchini kutokana na kifo cha aliyekuwa Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Salum Hassan Fereji. Anaripoti Yusuph Katimba…(endelea).

Sheikh Fereji alifariki dunia usiku wa kuamkia Julai 28 alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza kutokana na kusumnuliwa na ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu

Hayati Sheikh Fereji alifanyiwa ibada ya swala Julai 29, 2018 katika msikiti wa Raudhwa uliopo Mtaa wa Lumumba, Mwanza na kuzikwa siku hiyo hiyo.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na dini akiwemo Mufti wa Tanzania, Aboubakary Zubeir.

Salamu za pole za Rais Magufuli pia alizielekeza kwa Mufti Zubeir ambapo amesema, anamkumbuka Sheikh Fereji kwa ucha Mungu wake, ukarimu, upendo kwa wananchi na namna alivyokuwa akiunga mkono juhudi za kudumisha amani na kusukuma mbele maendeleo.

“Nimesikitishwa sana na kifo cha Sheikh Fereji, nilipokuwa nikienda Mwanza alikuwa miongoni mwa viongozi wa dini waliokuja kunipokea.

“Amekuwa akifanya kazi ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi makubwa na nchi yake, pole sana Mufti wa Tanzania na nakuomba unifikishie salamu zangu za pole kwa familia yake, Waislamu wote wa Mkoa wa Mwanza na nchi nzima pamoja na wote walioguswa na msiba huu,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!