Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aula SADC
Habari za Siasa

Rais Magufuli aula SADC

Rais John Magufuli
Spread the love

DK. John Magufuli, Rais wa Tanzania ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 18 Agosti, 2018 na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Rais Magufuli ameteuliwa na Wajumbe walioshiriki katika mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika Windhoek nchini Namibia kuanzia tarehe 17 hadi 18 Agosti mwaka huu.

Rais Magufuli atashikilia wadhifa huo kuanzia mwezi Agosti 2018 mpaka Agosti 2019.

Kufuatia uteuzi huo, Dk. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atapewa rasmi jukumu la Uenyekiti wa SADC katika Mkutano mkuu ujao wa 39 utakaofanyika Tanzania mwezi Agosti 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!