Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa Kenyatta
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa Kenyatta

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli ametuma salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta kufuatia shambulizi la kigaidi lililopoteza maisha ya watu 21. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Tukio hilo ambalo linatajwa kutekelezwa na kundi la kigaidi la Al-Shabaab, lilitokea katika hoteli ya DusitD2 iliyoko jijini Nairobi tarehe 15 Januari 2019, ambapo hadi sasa taarifa zinaeleza kuwa, watu 28 wamejeruhiwa huku wengine 19 wakipotea kusikojulikana.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Rais Magufuli amempa pole Rais Kenyatta kwa kuandika kuwa, “Punde nimezungumza na Mhe. Kenyatta kuhusu shambulizi la Jijini Nairobi, zaidi ya watu 14 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa. Pole sana Mhe. Rais na pole sana wananchi wa Kenya. Tupo nanyi katika kipindi hiki cha majonzi. Nawaombea Marehemu wote walale mahali pema peponi, Amina.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!