Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli atuma salamu za pole kwa Rais Kenyatta vifo vya watu 50
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli atuma salamu za pole kwa Rais Kenyatta vifo vya watu 50

Spread the love

RAIS John Magufuli ametuma salamu za pole kwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kufuatia vifo vya watu 50 vilivyosababishwa na ajali ya basi la abiria linalomlikiwa na kampuni ya Western Express Sacco Limited, lililokuwa likitokea jijini Nairobi kuelekea Kisumu nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Magufuli ametoa pole hizo katika ukurasa wake wa Twitter, kwa kuandika kuwa: “Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya basi iliyotokea Kericho nchini Kenya na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 50. Nakupa pole Rais Uhuru Kenyatta, familia za marehemu na Wakenya wote. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema na majeruhi wapone haraka. @UKenyatta.”

Ajali hiyo imetokea leo Jumatano alfajiri ya tarehe 10 Oktoba 2018, katika barabara ya Londiani-Muhuroni, Kaunti ya Kericho nchini Kenya.

Ajali hiyo ilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Kaunti ya Kericho, James Mogera ambapo alisema , miongoni mwa waliokutwa na mauti, ni watoto nane walio chini ya umri wa miaka mitano.

 Kamanda Mogera alisema, majeruhi waliokuwa katika basi hilo lenye uwezo wa kubeba abiria 67, wamepelekwa katika  Zahanati ya Fort Ternan na Hospitali ya Kaunti ya Muhoroni Sub kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa basi kuvamia reli kisha kupanda katika shamba la mawe na kuanguka chini mita 20.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!