Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ateua wakurugenzi watatu
Habari za Siasa

Rais Magufuli ateua wakurugenzi watatu

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakurugenzi watatu katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Mbeya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa imesema, uteuzi wa viongozi hao umeanza leo Jumamosi tarehe 4 Julai 2020.

Msigwa amesema, Rais Magufuli amemteua Anastazia Tutuba kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Mkoa wa Kilimanjaro.

Kabla ya uteuzi huo, Tutuba alikuwa Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Mkoa wa Arusha na anachukua nafasi ya Anna-Claire Shija.

Pili, Rais Magufuli amemteua Saad Mutambule kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Mkoa wa Arusha.

Kabla ya uteuzi huo, Mutambule alikuwa Afisa Mipango wa Jiji la Mbeya mkoani Mbeya na anachukua nafasi ya Alvera Ndabagoye ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Tatu, Rais Magufuli amemteua Elias Amede Ng’wanidako kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mbeya Mkoa wa Mbeya.

Kabla ya uteuzi huo, Ng’wanidako alikuwa Mweka Hazina wa Jiji la Mbeya na anachukua nafasi ya James Kasusura ambaye amestaafu.

“Wateule wote wanatakiwa kuwepo Ikulu, Chamwino Mkoa wa Dodoma tarehe 06 Julai, 2020 saa 4:00 asubuhi,” amesema Msigwa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!