Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Willy Komba kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (Teachers’ Service Commission – TSC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 8 Mei 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema uteuzi wa Dk. Komba umeanza leo.
Dk Komba ni Profesa Mshiriki wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na amechukua nafasi iliyoachwa na Oliver Mhaiki ambaye amemaliza muda wake.
Mhaiki aliongoza TSC kuanzia tarehe 27 Julai 2016 alipoapishwa na Rais Magufuli kushika wadhifa huo shughuli iliyofanyika Ikulu ndogo ya Chamwino jijini Dodoma.
Leave a comment