Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli ateua mrithi wa Jaji Nsekela
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli ateua mrithi wa Jaji Nsekela

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi, kuwa Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 23 Desemba 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa imesema Jaji Mwangesi ataapishwa kesho Alhamisi tarehe 24 Desemba mwaka huu, katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

“Rais Magufuli amemteua Mheshimiwa Mwangesi kuwa Kamishna wa Maadili. Uteuzi wake unaanza leo tarehe 23 Desemba 2020 na ataapishwa kesho tarehe 24 Desemba 2020 saa 4:00 asubuhi, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma,” imesema taarifa ya Msigwa.

Jaji Mwangesi anachukua nafasi ya aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Mstaafu, Haroid Nsekela, aliyefariki dunia tarehe 6 Desemba mwaka huu.

Marehemu Jaji Nsekela aliteuliwa na Rais Magufuli kuwa Kamishna wa Maadili katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, mwezi Desemba 2016 na alihudumu katika nafasi hiyo hadi umauti ulipomkuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!