RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Maduhu Isaac Kazi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Jumapili tarehe 12 Julai 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, kabla ya uteuzi huo, Dk. Kazi alikuwa meneja wa idara ya sera za kibajeti na madeni wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT).
Dk. Kazi anachukua nafasi ya Godffrey Idelphonce Mwambe.
Msigwa amesema, uteuzi wa Dk. Kazi unaanza leo tarehe 12 Julai, 2020.
Leave a comment