RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Eblate Ernest Mjingo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Jumanne tarehe 29 Septemba 2020 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, kabla ya uteuzi huo, Dkt. Mjingo alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Tiba ya Wanyamapori na Huduma za Maabara wa TAWIRI ambaye anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Simon Mduma ambaye amestaafu.
Msigwa amesema, uteuzi wa Dk. Mjingo unaanza leo Jumanne.
Leave a comment