Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Rais Magufuli apongezwa  
Afya

Rais Magufuli apongezwa  

Rais John Magufuli
Spread the love

SERIKALI inayoongozwa na Rais John Magufuli imepongezwa kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa kutoa na kuchukua hatua hasa katika magonjwa ya mlipuko. Anaandika Khalifa Abdallah… (endelea). 

Pongezi hizo zimetolewa na Kituo cha Kimataifa cha Kufuatilia, Kutathimini, Kutoa Taarifa na Kuchukua Hatua (CDC) kilichopo nchini Marekani.

Hayo yamesemwa na Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati wa kikao cha kuangalia hali ya utendaji katika sekta ya afya nchini.

“Wenzetu wa CDC kutoka Marekani wanatusaidia kujenga uwezo wa kufuatilia, kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa ya mlipuko kama vile Ebola na Kipindupindu na wameridhika kwa utendaji wetu hapa nchini,” amesema Waziri Ummy.

Amesema kuwa, Tanzania imeimarika katika kufanya uchunguzi, kutathimini,  kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa mbalimbali.

Mbali na hayo amesema  kuwa, magonjwa hayana mipaka hivyo ni lazima kuwa waangalifu na  kuchukua hatua mda wote kwa kujenga mifumo imara ya ufuatiliaji.

Inmi Petterson, Kaimu Balozi wa Marekani nchini amesema kuwa, wamefurahishwa na kazi ya wataalamu wa afya waliowekwa hapa nchini katika kupambana na magonjwa na kuahidi kuongeza nguvu kubwa ikiwemo vitendea kazi.

Aidha Balozi Inmi amesesema kuwa, Serikali ya Tanzania inatakiwa kushirikiana na wananchi wake katika kupata taarifa sahihi za magonjwa na kujenga nchi yenye wananchi wenye afya bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

AfyaBiashara

Meridianbet yatoa msaada zahanati ya Mwenge

Spread the love MABINGWA wa michezo ya kubashiri kampuni yaMeridianbet wamefanikiwa kufika eneo...

AfyaTangulizi

Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF

Spread the loveSERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Matende, mabusha tishio Kinondoni, wananchi waitwa kupata kinga tiba

Spread the loveMAGONJWA yasiyopewa kipaumbele ya Mabusha na Matende, bado yanaendelea kusumbua...

error: Content is protected !!